Natural Bliss

108. FAIDA ZA PROTEIN TREATMENT KWENYE NYWELE ASILIA (NATURAL HAIR)


📌Je katika ratiba zako za utunzaji nywele umewaza kuhusu kipengele cha matumizi ya Proteins? (Protein treatment au Protein Therapy).

Leo tutajifunza faida zake na nywele ikikosa lishe hii itakuaje.

Twende pamoja😊

Protein Treatment husaidia;

🧚‍♂️Kutunza unyevu na kuzifanya nywele kuwa nzito

-Mara nyingi nywele ikikosa protein huwa nyepesi sana na kupoteza ule uhalisia wake.

🧚‍♂️Husaidia kuziba mapengo yaliyowazi na kusaidia maeneo yaliyo yaliyodhoofika.

🧚‍♂️Kupunguza nywele kuwa nyembamba na kukatika ovyo

🧚‍♂️Kuimarisha nywele zilizoharibika kwa moto,rangi za nywele au Madawa(Relaxer)

🧚‍♂️Kuipa nywele kiwango sahihi cha protein na lishe kwa nywele zako

🧚‍♂️Kuzia nywele kubadilika rangi


📌Kumbuka kuzipa nywele zako proteins kabla na baada ya mitindo kinga hasa rasta au mitindo ya muda mrefu

📌Zingatia muda sahihi wa kuipa nywele zako protein ni kila wiki 4/6/8 inategemea na udhaifu ya nywele zako.


Je leo umefahamu kwanini nywele zako zinahitaji protein?au zikikosa protein zinakuaje?

Post a Comment

0 Comments